HALI ya maendeleo ya elimu wilaya ya Kiteto mkoani Manyara bado tete baada ya jamii kuendeleza kubariki ndoa za utotoni, mimba na utoro shuleni, huku siasa zikizidi kuathiri miradi mbalimbali ya maendeleo kwa jamii kusita kuchangia maendeleo hayo.
Mratibu wa Shirika lisilo la kiserikali la KINNAPA Bw.
Samuel Kerinja akitoa neno la awali kabla ya Ufunguzi wa mkutano
|
![]() |
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Nainge Lemalali akiugua mkutano wa wadau wa maendeleo wa Wilaya ya Kiteto mkoani |
Mwenyekiti wa Mkutano huo ambaye pia ni Mwneyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Nainge Lemalali alisema hali ya Wilaya ya Kiteto kimaendeleo ni bora ukilinganisha na awali kwani imepiga hatua kubwa.
“Ni kweli hali ni mbaya lakini ukilinganisha na miaka 10 iliyopita bado tunaamini hatua kubwa tumepiga licha ya mapungufu kadhaa yaliyomo…jambo la muhimu ni kuhakikisha tunasonga mbele kwa kushirikiana na si kutupiana lawama bila kutafuta suluhisho kwa pamoja”Alisema Lemalali.
Utafiti huo wa uwajibikaji ulifanywa na KINNAPA kwakushirikiana na Halmashauri ya Kiteto katika vijiji takribani 20 vya kata 13 kwa miaka miwili sasa wakiamini maendeleo huletwa na maarifa, ubunifu, mipango sahihi na bora, matumizi na usimamizi wa busara wa rasilimali zilizopo.
Mmoja wa wadau wa maendeleo
wilayani Kiteto Bw. Fratern Kwahhison akichagia mada katika mkutano huo
|
0 Comments