November 2013

viongozi wabainishwa kuwa chanzo cha migogoro ya wakulima na wafugaji



Na Said Njuki
WAKATI migogoro ya wakulima na wafugaji ikishika kasi nchini, Mashirika yasiyo ya kiserikali  (NGO's) mkoani Manyara yamedai kukithiri kwa migogoro hiyo kunatokana  na udhaifu wa uongozi bora na uwajibikaji kwa viongozi wa serikali.

Mashirika hayo yamedai kitendo cha migogoro hiyo kuibuka kila kona ya nchi ni aibu katika nchi inayotawaliwa kwa misingi ya utawala bora wakati viongozi wa serikali wa ngazi mbalimbali wapo kila kona, lakini kila taarifa za migogoro hiyo zimekuwa zikiripotiwa kila siku jambo ambalo ni hatari.

"Inasikitisha kusikia migogoro ya wafugaji na wakulima karibu kila kona ya nchi yetu,wakati viongozi wapo...matukio hayo ambayo mengine yanaambatana na mauaji huku wengine wakijeruhiwa na kubakia na vilema vya maisha ni vielelezo wazi kuwa upo udhaifu mkubwa wa utawala bora na uwajibikaji kwa viongozi wetu". Alisema  Mratibu wa mtandao wa mashirika hayo Mkoa wa Manayara (MACSNET) Bw. Nemence  Mabung'ai.

Bw. Mabung'ai alisema hayo katika mafunzo ya siku mbili ya wanachama wa mtandao huo juu ya jinsi ya mbinu za kuandika historia za miradi yenye mafanikio yaliyofanyiji mjini Babati Manyara na kuhudhuriwa na viongozi wa mashirika hayo zaidi ya 30 kutoka Wilaya za Babati, Kiteto, Simanjiro, Hanang na Mbulu.

" Serikali ya Tanzania ilishagawa kila eneo linamilikiwa na serikali za vijiji, Wilaya, Mkoa na taifa na  kila eneo linalo viongozi wa kuchaguliwa na kuteuliwa
...hata  hivyo bado maeneo mengi yenye viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya Kitongoji, kijiji, kata, Wilaya hadi Mkoa sheria,za ardhi zipo, lakini bado mapigano mengi  yanatokea  kwanini kama siyo uongozi mbovu na usiowajibika? " Alihoji Bw. Mabung'ai.

Alisema kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wamekuwa wakipambana na hali hiyo kwa muda mrefu kwa kutoa elimu na kwamba kinachokwamisha kwa kiasi kikubwa ni viongozi hao kutowajibika ipasavyo na kwamba mifumo ya uongozi na uwajibikaji ingetekelezwa vizuri migogoro hiyo ingefikia mwisho.

Alishauri viongozi wenye maeneo yenye migogoro hiyo wakae pamoja na wadau husika kupanga kuweka mipango ya matumizi bora ya ardhi na kusimamia mipaka hiyo, tofauti na hilo migogoro haitaosha nchii.

Kiongozi wa Shirika lisilo la kiserikali la  Hanang Wemen Concelling Development  Association (HAOCODA) Bi. Rose Tippe alisema tatizo ni utendaji mbovu kwa wasimamizi wa sheria, lakini bado mashirika hao yanafanya kazi kubwa ya na yanastahiki pongezi kwa jitihada zao katika kupigania haki za wafugaji na wakulima hao



WANAFUNZI 48 WA SHULE YA KIISLAM YA CHAMANZI WAHITIM MAFUNZO YA SKAUTI


baadhi ya skauti wakitoka katika uchunguzi wa shughuli  za kijamii katika tasisi mbalimbali kama polisi , sokoni, n.k, kama sehem ya mafunzo yao
skauti wakisikiliza maelezo ya mkufunzi wao baada ya kutoka katika shughuli za kijamii
Na Said Njuki Dar es Salaam

SKAUTI 48 wa Shule ya Msingi ya Kiislamu ya Chamazi wamepata mafunzo ya kijasiri kwa lengo la kuwajenga kikakamavu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kujitegemea kimaisha.

"Malengo hasa ni  kumwandaa vijana w awe wakakamavu, jasiri waweze  kujitegemea na hatimaye wawe ni msaada kwa jamii ikiwa ni pamoja na kujiandaa kiakili kiutafiti kwa faida ya yake, na taifa". Alisema Alhaj Omari Mavura Kamisha Msaidizi Skauti Makao Makuu.

Mavura alisema hiyo ni kambi ya Kwanza ya aina yake, ambapo wasichana 27 na wa vulana 21 na ilikuwa  ya siku nne ambapo vijana hao wenye umri kati ya miaka saba na 12 waliweza kufanya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ulinzi wa maeneo yao.

Naye mkufunzi wa mafunzo hayo Bw. Mustafa Musoma alisema kwa kawaida mafunzo hayo  hufanyika mara nne kwa mwaka ambapo mwezi wa  Desemba mwaka huu yatafanyika tena ili kwenda sambamba na mtazamo wa Shule wa kuwaandaa vijana kikakamavu.

Mkuu wa Shule hiyo Bw. Abdallah Ngorini alisema viongozi wa Shule hiyo hufarijika sana hasa vijana wanapofnya mazoezi kama hayo ni kujiweka vizuri kiafya na kiakili.

Wakufunzi wengine ni Dotto Mohamed na Abdulrahim Nassoro wa Markaz Gongolamboto.
tunakunywa chai baada ya kutoka katika mafunzo na shughuli hizo.


MWANAMKE WA BABATI ALIYEKUFA KIFO TATA KATIKA SAKATA LA OPERESHENI TOKOMEZA UJANGILI AZIKWA WIKI 3 BAADA YA KIFO CHAKE CHA KIKATILI

mwili wa marehemu Emiliana anaedaiwa kuuawa na askari wa hifadhi ya TANAPA ukiwa kanisani katika ibada maalum ya kumuombea Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi
Na Said Njuki Babati


MWANAMKE  Emiliana Maro (42) aliyekuwa  kifo cha utata baada ya kuchukuliwa na timu ya Operesheni Tokomeza Ujangili wiki tatu zilizopita amezikwa juzi Jumamosi kijiji cha Oringadida  kata ya Qash Wilaya ya Babati mkoani Manyara.

Katika mazishi hayo yaliyohudhuriwa na umati mkubwa wa watu kutoka pembe zote za Wilaya ya Babati na nje ya Wilaya hiyo,  hakuna kiongozi wa serikali wa ngazi ya Wilaya na Mkoa aliyehudhuria mbali na viongozi wa vyama vya Siasa  akiwemo mbunge wa Babati vijijini Bw. Jitu Soni  (CCM), Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wolaya ya Babati vijijini Bw. Nicodemus Tarimo huku  CHADEMA wakitumia  wawakilishi.
Baadhi ya wanafamilia wa marehem Emiliana Kibuga wakihuzunika kwa kifo tata cha ndugu yao inayodaiwa kusababishwa na askari wa Tarangire
Inadaiwa marehemu  Emiliana alichukuliwa na timu hiyo Oktoba 16 asubuhi ambapo jioni alirudishwa na askari hao akiwa taabani kwa ajili ya upekuzi  huku watoto wake Shaabani na Morgan wakiwa kwenye ulinzi mkali na kisha kuondoka naye tena hadi walipopiqiwa simu na Polisi wakitakiwa kuchukua mwili wa mtuhumiwa huyo.
mmoja wa watoto wa marehem Emiliana Kibuga akiuaga mwili wa mama yake mzazi
Awali, kabla ya mazishi hayo pikipiki zaidi ya 200 na gari 70 za Kata hizo zilisitisha kazi kwa ajili ya kwenda kuchukua na kuusindiki-mwili wa marehemu toka mochwari ya hospitali ya Mrara mjini Babati hadi nyumbani, huku wasindikizaji hao wakiwa na mapango yenye ujumla mbalimbali.

Baadhi tu yaliandikwa ' Lini mwanamke akauwa tembo? Paki (TANAPA) marufuku kukanyaga Galapo na mwaka 2015 tembo waende kupiga kura'
huku wakilaani waliohusika na mauaji hayo.

Paroko wa Kanisa Katoliki Galapo Baba Eugene Kubasu akiongoza Ibada aliitaka serikali kuhakikisha waliofanya unyama huo wanabainika na kuchukuliwa hatua za kisheria na wao na wananchi kwa ujumla wapiga magoti wakimshitakia Mwenyezi Mungu haki itendeke na si vinginevyo.

Mwakilishi wa Kamati ya mazishi Bw. Jumanne Mwanja akisoma wasifu wa marehemu kwa niaba ya familia alisema kwa mujibu wa mume wa marehemu huyo Bw. Elias Kibuga mke wake hakuwa na magonjwa ng'ang'anizi kama shinikizo la damu, sukari au vidonda vya tumbo, amekuwa akiugua magonjwa yenye kutibika kwa urahisi.

Pia familia hiyo ilieleza kuwa kitendo kilichofanywa na timu ya Oporesheni Tokomeza Ujangili dhidi ya mwanamke huyo na wengine nchini katika kipindi hicho ni ukiukaji wa sheria za nchi hivyo kuiomba serikali kuchukua hatua wahusika bila kuwaonea haya.
Mbunge wa jimbo hilo bwana Jitu akiweka shada la maua katika kaburi la Emiliana Kibuga anaedaiwa kuuawa na askari wa Tarangire
Mbunge wa Babati vijijini Bw. Jitu alisema tukio hilo limewasikitisha sana kama wabunge na kuahidi kwamba wabunge wote wa Mkoa wa Manyara watahakikisha sheria inashika mkondo wake.

Hata hivyo licha ya umma kufurika kuuaga mwili huo huku wengi wao wakitamani kushuhudia uso wa marehemu, familia ilikataa kata kata kuweka uso wazi kwa madai ya sababu maalumu.
mume wa marehemu Emiliana Kibuga akiuaga mwili wa mkewe  huku akinyanyua hadi picha hiyo kwa huzuni kubwa baada ya kuachiwa ambaye nae alitekwa kabla ya mkewe na askari hao lakini baadae kuachiwa baada ya mkewe kuuawa
Add caption
Wananchi kwa uapnde wao walilazimisha kufunguliwa kwa mwili huo, hadi Kiongozi wa Kamati ya mazishi na musemaji wa familia Bw. Godwin Sanda alipowasihi wananchi hao kukubaliana na uamuzi huo.
majirani, ndugu jamaa na marafiki wa familia ya Emiliana kibuga wakiuaga mwili wa mpendwa wao



hatimaye mwili wa Emiliana umezikwa,

NJUKI BLOG INAWAPA POLE  WOTE WALIOGUSWA NA MSIBA HUO
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEM EMILIANA MAHALA PEMA PEPONI
AMINA

Newer Posts Older Posts