KONDOA WILAYA KONGWE YENYE MIUNDO MBINU 'BUTU' NA MAISHA DUNI


Daraja hili halijawahi kupitisha gari kwa miaka kadhaa sasa, lakini limekuwa likijengwa karibu kila mwaka na kabomolewa na maji ya mbua...sijui kulikoni...na sijui fedha za ujenzi zinapatikana wapi! Daraja hili lipo kijiji cha Itiso barabara ya Kondoa-Bolisa.
Daraja la Kolo, Kondoa, hivi viongozi hawakuliona hilo miaka yote hiyo? Tushukuru Mwenyezi Mungu barabara hiyo sasa itajengwa kwa kiwango cha lami huenda ndio suluhisho la magari kupitia korongoni miaka yote  
Darasa la Kolo katika barabara ya Dodoma-Arusha, lilivunjika miaka zaidi ya 15 iliyopita hadi leo halijajengwa, lingekuwa na Sarenda Dar es salaam, Karanga Moshi au Nduruma Arusha ingekuweje?

WILAYA ya Kondoa mkoani Dodoma ni moja ya Wilaya kongwe nchini, inasadikiwa Iliana rasmi miaka 87 iliyopita, ikiwa ni miaka 35 kabla ya Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 na miaka 52 baada ya uhuru huo, yaani ilihali wa rasmi mwaka 1926.

Makao ya Makuu ya Wilaya hii inaaminika ndipo yalipokuwa Makao Makuu ya Jimbo la kanda ya Kati (Central Province) lilojumuisha Meiji mikuu ya Dodoma, Mpwapwa na Singida wakati huo,ambapo wakoloni wa Kijerumani wapokea kodi za mababu zetu mjini Kondoa pamoja na mikusanyiko na maamuzi yote ya utawala wa kikoloni ilifanyika hapo.

Jengo hili hapa chini linalosadikiwa kuwa iliojengwa mwaka 1902 na Wakoloni hao wa Kijerumani kwa nguvu za watanganyika wakati huo. Sasa jengo hilo linatumika kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kondoa na Ofisi zingine.




Wilaya hii licha ya ukongwe huo barabara iliyojengwa kwa kiwango cha lami ni kilomita tatu, tu kati ya tano zilizoahidiwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa safari zake Dkt. Jakaya Kikwete kati ya kilomita zaidi ya 800 za barabara wilayani hapa.

Lakini licha ya barabara ndefu na muhimu barani Afrika inayotoka Cape Town Afrika ya Kusini hadi Cairo Misri kupitia wilayani Kondoa na Chemba kwa zaidi ya kilomita 170 ndiyo kipande kilichobaki kirefu hakijajengwa kwa kiwango cha lami jambo linalokwamisha maendeleo ya wananchi wa eneo hili.
 

Newer Post Older Post

Leave a Reply