WANAFUNZI 48 WA SHULE YA KIISLAM YA CHAMANZI WAHITIM MAFUNZO YA SKAUTI


baadhi ya skauti wakitoka katika uchunguzi wa shughuli  za kijamii katika tasisi mbalimbali kama polisi , sokoni, n.k, kama sehem ya mafunzo yao
skauti wakisikiliza maelezo ya mkufunzi wao baada ya kutoka katika shughuli za kijamii
Na Said Njuki Dar es Salaam

SKAUTI 48 wa Shule ya Msingi ya Kiislamu ya Chamazi wamepata mafunzo ya kijasiri kwa lengo la kuwajenga kikakamavu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kujitegemea kimaisha.

"Malengo hasa ni  kumwandaa vijana w awe wakakamavu, jasiri waweze  kujitegemea na hatimaye wawe ni msaada kwa jamii ikiwa ni pamoja na kujiandaa kiakili kiutafiti kwa faida ya yake, na taifa". Alisema Alhaj Omari Mavura Kamisha Msaidizi Skauti Makao Makuu.

Mavura alisema hiyo ni kambi ya Kwanza ya aina yake, ambapo wasichana 27 na wa vulana 21 na ilikuwa  ya siku nne ambapo vijana hao wenye umri kati ya miaka saba na 12 waliweza kufanya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ulinzi wa maeneo yao.

Naye mkufunzi wa mafunzo hayo Bw. Mustafa Musoma alisema kwa kawaida mafunzo hayo  hufanyika mara nne kwa mwaka ambapo mwezi wa  Desemba mwaka huu yatafanyika tena ili kwenda sambamba na mtazamo wa Shule wa kuwaandaa vijana kikakamavu.

Mkuu wa Shule hiyo Bw. Abdallah Ngorini alisema viongozi wa Shule hiyo hufarijika sana hasa vijana wanapofnya mazoezi kama hayo ni kujiweka vizuri kiafya na kiakili.

Wakufunzi wengine ni Dotto Mohamed na Abdulrahim Nassoro wa Markaz Gongolamboto.
tunakunywa chai baada ya kutoka katika mafunzo na shughuli hizo.


Newer Post Older Post

Leave a Reply